MCHUNGAJI AIMANA DOMINICK
SOMO: YEYE NI MUNGU WA YASIYOWEZEKANA
Mungu tunayemtumikia na kumwabudu ni Mungu wa yasiyowezekana, hii inamaana kuwa YEYE sio Mungu wa mambo madogo. Je! Unaamini kuwa Mungu unayemwabudu ni Mungu wa yasiyowezekana?
Ezra 1:2-3 “Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi; Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya Bwana, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu.”
Mungu wa Mbinguni aliusukuma moyo wa Koreshi mfalme wa wajemi kuijenga nyumba ya Bwana, huyu Mungu anayeweza kufanya yasiyowezekana alisimama na Wayahudi wote wakajenga nyumba ya kumwabudu Mungu.
Mungu anayeweza kufanya mambo yasiyowezekana alisimama pamoja na wayahudi na kujenga nyumba ya Bwana, alionyesha nguvu zake pale alipomuagiza Mfalme wa Uajemi kumjengea nyumba kwa ajili ya wana wa Israeli. Katika nyakati zetu hizi Mungu wa Mbinguni amemuagiza mtumishi wake Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira amjengee nyumba katika Efatha lililo taifa lake. Kama vile ambavyo Uajemi lilikuwa taifa lenye nguvu ndivyo ambavyo Mungu wa Mbinguni ameifanya Efatha kuwa taifa lake lenye nguvu, lenye uweza na mamlaka, lenye upendeleo maalumu wa kiungu na la kutetemekewa na kutamkwa popote pale.
Mimi na wewe tumechaguliwa tuwe Taifa kuu na Takatifu, Bwana ametufanya kuwa taifa kuu na hodari na kupitia sisi mataifa yote yatabarikiwa, Lazima uonyeshe kuwa wewe ni taifa kuu na hodari hivyo usifanye mambo kwa ulegevu.
... See MoreSee Less