NENO LA SIKU.
Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira- Kanisa la Efatha.
TAREHE 07/02/2025.
SOMO: TAMANI KUWA UTUKUFU WA MUNGU.
Yesu anakupenda alikufa kwa ajili yako, alilipa gharama ya thamani mno, alitoa Uhai wake ili upokee msamaha toka Mungu ili kwamba uweze kuwa Mwana wa Mungu. Hakuna aliyelipa gharama kwa ajili yako kama Yesu alivyofanya, acha nasi tuwe kwa ajili yake.
Ukifika kiwango hiki cha Imani, chochote utendacho, usemacho, ulichonacho, unacho miliki na chochote uwazacho ni kwa ajili ya Utukufu wa Mungu. Chochote uwazacho ni kumfanya Mungu atukuke maana yake ni kuwa wewe na maisha yako unakuwa ni kwa ajili ya kumuinua Mungu.
Yusufu alipofika katika nyumba ya Potifa chochote alichofanya au kusema kilikuwa ni kwa ajili ya kumuinua Mungu mpaka Potifa akamkabidhi kila kitu kwa sababu alitambua kuwa hata Ustawi aliokuwa nao ni kwa sababu yake. Unaweza ukawa ni dada msaidizi wa kazi za nyumbani kwa mtu au unafanya kazi mahali katika kampuni ya mtu na kupitia wewe hiyo kampuni inastawi, kwa nini? Kwa sababu maisha yako si yako tena bali ni kwa ajili ya Utukufu wa Mungu.
Yusufu hata alipokuwa mfungwa alionyesha kuwa yeye japo ni mfungwa lakini Utukufu wa Mungu upo naye bado na kwa sababu hiyo alifanya vizuri.
Mwana wa Mungu kuanzia leo, utafikia kiwango hicho nina amini kwa moyo wangu wote, kwa Jina la Yesu hakuna kitakacho kuzuilia kufika hapo.
... See MoreSee Less